
NYIMBO KWA UTUKUFU WA MUNGU
Kimara Seventh -Day Adventist Church
P.O. BOX 12894, DSM, TANZANIA
Eastern Tanzania Conference (ETC)
MATANGAZO YA KANISA
BUL/KIM/SDAC/36/2014
SABATO YA TAREHE 06/09/2014

WAHUDUMU SABATO YA TAREHE 13/09/2014
Mhubiri Kwa Watu Wazima: Mwinjilisti Mwandambo
Mwenyekiti: F. Majanjara
Fungu Kuu Na Ombi: J. Yona
Zaka Na Sadaka: T. Kilimo
Watoto: E. Kileng'a
Mashemasi: Wote
Wazee Wa Zamu: E. Kisika & G. Makoko
-
Sabato ijayo ya tar 13/09/2014 itakuwa ni Sabato maalumu ya changizo kwa ajili ya umaliziaji wa Kanisa letu ili kuwekwa wakfu mwaka huu, hivyo waumini wote tuweze kujiandaa kwa ajili ya Sabato hiyo kwa kumtolea Mungu. Lengo katika Sabato hiyo ni kupata kiasi cha shilingi 33,000,000,00.
-
Tunaendelea kuwatangazia juu ya mkutano wa Vijana utakaofanyika katika Chuo cha Baraton Nchini Kenya mwezi Disemba, 2014. Kiingilio ni USD 100 ambazo kwa Makadirio ni kama Tsh 170,000/=. Na mwisho wa kutoa kiingilio ni Septemba. Kwa yeyote anayehitaji kwenda, aonane na kiongozi wa vijana Kanisa la Kimara- Sharon Nyuki.
-
Program ya chakula inapatikana Kanisani Kimara kwa gharama ya Tsh 1500/=. Inasisitizwa kuwa kwa wote wanaohitaji watoe fedha yao mapema na siyo siku ya Sabato.
-
Sabato ya tarehe 13/09/2014 kwenye program za mchana kutakuwa na Semina ya Shule ya Sabato itakayofanyika Kanisani Kimara.
-
Sabato ya Tarehe 20/09/2014 kutakuwa na Meza ya BWANA. Waumini tujiandae kwa Sabato hiyo.
-
Kutakuwa na Kapu la Tumaini Sabato ya terehe 27/09/2014, waumini wote tuweze kujiandaa kwa Sabato hiyo.
-
Kutakuwa na Dawati la afya litakaloanza wiki hii. Kila siku za Ibada yaani maombi ya asubuhi jumapili, maombi ya jumatano, kufungua Sabato na Ibada ya Jumamosi kutakuwa na mtaalamu wa Afya ambaye atakuwa zamu kwa huduma ya dharura itakayojitokeza. Hivyo basi kama utakuwa na tatizo lolote la kiafya utamuona mhudumu huyo ambaye atakuwa zamu.